Monday, June 9, 2014

COMING SOON ON 13TH JULY 2014......LAUGH AGAIN CONCERT....Chavala Hatimaye!!!!

 Siku utakayoanza kupambana na Opinions za watu kuhusu wewe na ukasahau kuwa unazo Facts za kutosha kuhusu wewe mwenyewe, hapo ndio utakuwa umeacha kuishi maisha yako halisi na umeanza kuishi maigizo!!

Ukijitambua sawa sawa hutajitahidi kuishi ukiwaonyesha watu jinsi uishivyo ila utajitahidi kumpendeza Mungu na walimwengu sawa sawa na vipimio vya ki-Mungu!! Unapombana na binadamu mwenzio kwa sababu yeyote ile inaonesha kuwa wewe ni MUOGA na unadhani kupambana na wengine ndio kunaweza kukufanya uwe juu, Au huna jambo la maana la kufanya na ndio maana unapata hata muda wa kupambana na wenzio na Au ni Ujinga tu uliochanganyikana na utoto ambao mpaka ukutoke itachukua muda sana!!

Yaani kupigana au kushindana na mwenzio ni sawa na kijiko kiwe na ugomvi na uma au sahani igombane na flampeni kabatini la vyombo hali vyote viko chini ya mwenye nyumba na kila kimoja kimenunuliwa kwa kazi yake na mwenye navyo ndio huamua kipi kifanye nini,kikae wapi na kitupwe lini....sisi sote ni uumbaji wa Mungu,sasa tusemane au kupigana au kushindana ili iweje????/

Nina mengi sana ya kufanya na maisha yangu,yako mengi yananingoja kutimiza na naona muda hata haunitoshi, Ahsante mungu kwa afya njema na akili timamu na msimamo wenye nidhamu katika wewe!







MUHIMU KWA KILA MT:
Tumia muda wako vema na kila siku fanya bidii kutimiza ndoto zako, dini na ujinga havitakufikisha popote, hebu jitafakari tena unatumiaje muda wako!! na ukiona unatumia muda mrefu kufuatilia sijui nani kafanya nini na unatamani kama ungepambana basi ujue una matatizo na ukiendelea hivyo utapotea na kusahaulika kabisa!!!!

Serious people have serious issues to deal with and not other people!!

Think outside the box and be Yourself!!