Tuesday, August 6, 2013

HALI NI MBAYA SANA KWA WATOTO YATIMA WA HOCET,TAFADHALI MSAADA WAKO UNAHUSIKA SANA!!!

SHALOM!
HABARI ZENU WAPENDWA!!
NINAAMINI MNA MOYO WA UPENDO, TENA WA KUWAJALI WENGINE KULIKO NINYI, NA HATA ZAIDI BIBLIA INASEMA UPENDO WA KWELI NI ULE WA KUWAPENDA WENGINE ZAIDI.
*****HANANASIFU ORPHANAGE CENTRE (HOCET)....HAWANA CHAKULA KABISAAAAA NA WEWE NA MIMI PEKEE NDIO TUNAWEZA KUWALISHA KWA SIKU 120, KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA****
LEO NINALO OMBI MAALUM KWENU, NI MUHIMU SANA SANA....KUNA KITUO KIMOJA CHA KULELEA WATOTO YATIMA (WATOTO WA MUNGU), KITUO KINACHOENDESHWA NA WATU TU WALIOJITOLEA, NA HAPO AWALI KILIKUWAQ KINAFADHILIWA NA WAZUNGU FULANI, LAKINI BAADA YA KUONA WATOTO HAO WAMEKAZANA NA MUNGU NA HAO WAZUNGU (WAFADHILI) WAKAWEKA MASHARTI, ETI KAMA WAKITAKA WAENDELEE KUPOKEA MISAADA YAO BASI WAACHANE NA HAYO MAMBO YA YESU YESU....NA KWA KUWA HAKUNA BABA MWINGINE ZAIDI YA MBINGUNI NA HAKUNA  NAMNA BINADAMU ANAWEZA KUISHI KWA MISAADA YA BINADAMU MWINGINE BAADA YA KUMKANA MUNGU WA KWELI.
 
SASA WATOTO HAO WAKO KWENYE ENEO LAO LA SHULE WANASOMA NA WANAYO MIRADI AMBAYO BADO HAIJAANZA KULETA FAIDA ILI WAWEZE KUJIENDESHA WENYEWE, NAHIYO ITAKUWA HIVYO TU BAADA YA MIEZI MITATU AU MINNE KUANZAIA SASA.
WATOTO HAWA KWA SASA HAWANA CHAKULA KABISA, NA HATA LEO WAMEKULA KWA MSAADA WA KIJANA MMOJA ALIJITOLEA YEYE BINAFSI NA FAMILIA YAKE....MBALI NA GHARAMA NYINGINE ZA UENDESHAJI KAMA MISHAHARA/POSHO ZA WALIMU;
************************************************************************************************
KITUO HIKI KINATUMIA UNGA KILO 30, MAHARAGE KILO 14 NA SUKARI KILO 5....NA IKIWA NI WALI,BASI HUHITAJIKA KILO 30 ZA MCHELE KWA MLO MMOJA....NA PIA UNAWEZA KUCHANGIA MAFUTA NA FEDHA KWA AJILI YA VITU VINGINE VINAVYOWEZA KUHITAJIKA.
************************************************************************************************

NINAAMINI KWA MSAADA WA WATANZANIA WOTE WENYE MAPENZI MEMA NA WATOTO WA KITANZANIA, WATOTO HAWA HAWATAKOSA CHAKULA KWA SIKU HIZI 120 ZA MPITO KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA WENYEWE, SIO LAZIMA ULETE MSAADA MKUBWA SANA, LAKINI NAAMINI UNAWEZA UKAJITOLEA CHAKULA KIASI JAPO KWA SIKU MOJA TU KAMA SIO TATU, YAWEZA KUWA WEWE BINAFSI AU KAMPUNI AU FAMILIA AU KANISA, LAKINI NINACHOKIAMINI NI KUWA KAMA KWELI TUNAAMINISHA KUMPENDA MUNGU NA KUWAPENDA WATOTO WATANZANIA TENA WANAOLELEWA KATIKA MALEZI YA KIMUNGU BASI LAZIMA WATOTO HAWA WATAISHI BILA HOFU YA CHAKULA KWA SIMU HIZI 120, NA KWA HAKIKA BWANA ATAKUBARIKI SAWASAWA NA IMANI YAKO KWAKE
YAK 1:27 "....DINI ILIYO SAFI ISIYO NA TAKA MBELE ZA MUNGUBABA NI HII, KUWATAZAMA WAJANE NA YATIMA KATIKA DHIKI YAO NA KUJILINDA NA DUNIA PASIPO NA MAWAA"
 
MSAADA HUO UNAHITAJIKA SANA SANA, NAAM KWA NAMNA YOYOTE ILE UNAYOWEZA KUCHANGIA BASI USISITE,FANYA HIVYO...SADAKA YAKO YA KUWALISHA WATOTO HAWA HAITASAHAULIKA HATA KIDOGO, UNAWEZA KULETA MCHANGO WAKO WA CHAKULA PALE OFISI ZA NIIM COMPUTERS, MOROCO HOTEL AU UKATUMA MCHANGO WAKO WA FEDHA KWA NJIA YA SIMU, NAAM KWA MAULIZO ZAIDI 
TAFADHALI WASILIANA NA WASIMAMIZI NA WARATIBU WA ZOEZI HILI KWA NO.
0713 26 1425 na 0754 527955, pia 0783 757051
KWA NIABA YA WASIMAMIZI WA KITUO HIKI NINAWASHUKURU HATA KABLA HAMJAFANYA JAMBO LOLOTE MAANA NAAMINI UMEGUSWA NA UKO TAYARI SASA KUWASAIDIA WATOTO HAWA...KAMA TUNAWEZA KUCHANGIA SHEREHE ZA HARUSI, NAFIKIRI HATMA YA WATOTO HAWA NI ZAIDI,MUNGU AKUBARIKI UNAPOMSHIRIKISHA NA MWENZAKO!!
 
Imeandikwa na
KING CHAVALA MC
KWA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.

Saturday, August 3, 2013

NINAMSHUKURU MUNGU SANA KWA UPENDELEO ALIONIPA.....JANA NILIKUWA MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI YA CHUO CHA UTABIBU,KIBAHA!!!

HABARI ZENU!
NINAMSHUKURU MUNGU SANA SANA KWA UPENDELEO NILIOUPATA NA ANAOENDELEA KUNIPATIA KILA SIKU.

JAPO NIMEKUWA KIMYA KWA KIASI LAKINI NIMEKUWA NA MAMBO MENGI SANA YANAYOENDELEA CHINICHINI.

NINAMSHUKURU MUNGU TANGU NIMEANZISHA MPANGO MAALUM WA KUWASAIDIA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KUJITAMBUA, SASA TUMEFIKA MAHALI FULANI NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE,MPAKA SASA NIMESHAFANYA PROGRAM NNE; NA NAAMINI WOTE WALIOFANIKIWA KUHUDHURIA WAMEFAIDIKA SANA NA MAFUNZO YA HUKO.

NA MWEZI WA KUMI NITAZINDUA PROGRAM NYINGINE AMBAYO ITAKUWA INAWAHUSISHA WASICHANA WENYE VIPAJI VYOTE VYA ASILI NA MFULULIZO WA MATAMASHA HAYA UTAITWA "LADIES TALENT BATTLE"...Battling against Evil for the sake of the Kingdom!!....WASICHANA WOTE STAY TUNED!!!

LAKINI PIA NINAMSHUKURU SANA MUNGU KUPATA NAFASI YA KUWASILISHA AU KUSEMA KUPITIA VYOMBO VYA HABARI....KARIBUNI NIMEKUWA ITV, KISHA TBC 1 NA PIA MWANANCHI NA ZAIDI NINACHO KIBALI CHA KUENDELEA KUONEKANA KATIKA VYOMBO VYA HABARI VINGINE.....FURAHA YANGU SIO KUONEKANA TU,BALI NAFURAHI KWASABABU MUNGU AMERUHUSU NISEME, NIFUNDISHE NA KUWAFURAHISHA NA WALE WENGI WALIO MBALI DUNIANI KOTE!

JANA IJUMAA NILIALIKWA KAMA MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI YA WANAFUNZI WA UTABIBU WA KIBAHA-COTC (CHUO KIKO NDANI YA HOSPITALI YA TUMBI),WANAFUNZI WALIOSOMA DIPLOMA YAO KWA MIAKA MITATU SASA WANAJIANDAA KUWA MATABIBU HUKO TANZANIA KOTE...HII NI FAMILIA YA TAFES NA KWA HAKIKA SHEREHE HIYO ILIKUWA NZURI SANA!

NILIBAHATIKA KUONANA NA WATU WENGI,WAZAZI WALEZI WA WANAFUNZI HAO NA NAMSHANGAA MUNGU KWA KIBALI NILICHOKIPATA MBELE YA MACHO YAO NA MIOYO YAO!

NA JUMAMOSI MCHANA NITAKUWA SAFARINI KWENDA DODOMA, KESHO NITAKUWA NINAONGEA VIONGOZI VIJANA KATIKA SEMINA YA UONGOZI ILIOANDALIWA NA YKM NA BADO NINAMSHUKURU MUNGU SANA KWA UPENDELEO HUO!!

NATAMANI KATIKA KILA NINALOFANYA JINA LAKE NA YEYE AHESHIMIWE SANA KULIKO KINGINE CHOCHOTE, NAAM NA ANIPE UNYENYEKEVU ILI KAMWE NISIJISIFU WALA KUJIINUA,KWA WALE WALIO ULIMWENGU MWINGINE WATAGUNDUA HII KUWA...UKIWA NA YEYE BASI UNA KILA KITU,AMEN!!

aHSANTENI SANA,MUNGU AWABARIKI,NINAWAPENDA SANA NINYI NYOOOOTE!!
MLIO WA KWELI BASI MSIACHE KUNIOMBEA KILA SIKU!!

Na 
KING CHAVALA
MC/STAND UP COMEDIAN
+255 713 883 797
Facebook; King Chavala MC
Twitter; kingchavala

Friday, August 2, 2013

CHEKA TENA NA KING CHAVALA.....NGOMA DROO KATI YA BOSI NA HOUSEBOY!!!

HABARI ZENU TENA MARAFIKI ZANGU NYOTE!!
LEO TENA WAKATI NAPANGA NA KUPANGUA MAFILE YANGU NIMEKUTANA NA CLIP HII AMBAYO NILIIFANYA NIKIWA HOME LIKE TWO YEARS BACK!!

NA HII NI HABARI INAYOMHUSISHA BOSSI MMOJA ALIYEKUWA NA MKE NA WATOTO NA PIA ALIKUWA AMEAJIRI WAFANYAKAZI WA NDANI HOUSEBOY(BARAKA) NA HOUSEGIRL(FARAJA);

BOSI ALIKUWA NA TABIA YA KUDOKOA DOKOA NJE YA NDOA NA IKATOKEA AKADOKOA MPAKA HOUSEGIRL, BINTI AMBAYE HOUSEBOY NAYE ALIKUWA AKIMEZEA MATE,NA BAHATI MBAYA YULE BINTI AKAPATA UJAUZITO, MAMA MOJA KWA MOJA AKAMUHISI BARAKA KUHUSIKA LAKINI AKAWA AMEMEZEA KWANZA KUSUBIRI SAA MUAFAKA YA KUMWEKA KITAKO.

YULE BOSI ALIKUWA ANAPENDA SANA WINE, NA BARAKA ALIKUWA NA TABIA YA KUNYWA WINE YA BOSI WAKE BILA KUOMBA NA KILA ALIPOKUWA AKICHUKUA ALIONGEZA MAJI ILI KIMO KIBAKI PALEPALE.

BASI KUNA WAKATI BOSI ALITAFUTA MBINU NA AKABAHATIKA; ALINUNUA WINE AMBAYO AKITIA TU MAJI INABADILIKA RANGI.....BASI BARAKA KAMA ILIVYO ADA AKAJA NA KUMIMINA NA KISHA KUTIA MAJI,SASA ALIPOTIA MAJI TU MARA IKABADILIKA RANGI NA MCHANA HUOHUO BOSI AKAREJEA NYUMBANI NA MKEWE TOKA MATEMBEZINI NA KUKUTA WINE IMEBADILIKA RANGI, BASI YULE BOSI NA MKEWE WAKAKAA SEBULENI NA KUPUMZIKA NA YULE BOSI AKAITA KWA NGUVU BARAKA ALIYEKUWA JIKONI NA MAZUNGUMZO YAO YALIKUWA HIVI;

BOSI; BARAAAAAAKA
BARAKA; NAAM BOSI!
BOSI; NI NANI ALIYEKUNYWA WINE YANGU?
BARAKA; (KIMYA)
BOSI; (AKARUDIA KUITA MPAKA MARA TATU NA KUULIZA)
BARAKA;(NAE AKAITIKA KILA ALIPOITWA ILA HAKUJIBU NENO PALE ALIPOULIZWA)
.....Mara Baraka akakimbia na kuja sebuleni na kusema bosi samahani,yaani ukiwa jikoni,ukiwa umevaa hii na ukiwa unakatakata karoti,husikii kitu chochote isipokuwa jina lako tu ukiitwa,kama huamini na wewe nenda uone
(Basi Mama na Baraka wakamsonga kwa vituko mpaka Bosi nae akavaa epron kwa hasira na kwenda jikoni ili tu athibitishe na akirudi amfute kazi kabisa Baraka)
Basi na Baraka nae akaita....

BARAKA; BOOOOOOSI
BOSI; YES BARAKA!
BARAKA; NI NANI ALIYEMPA UJAUZITO FARAJA?
BOSI;(KIMYA)
BARAKA; (AKAITA TENA NA TENA KWA MBWEMBWE)
BOSI; (NAE AKAITIKA JINA NA KUKAA KIMYA)

Na hapo bosi akarudi kwa kasi sana sebuleni na kusema ni kweli aisee,Baraka nenda kaendelee na kazi tu......Basi akitaka kuondoka akamuuliza mama na wewe unataka kuhakikisha haya

MMMhh MAMA AKASEMA AKHUUU! (Maana anajua mabaya yake yanajulikana na houseboy)

hahahahahaha Cheka na ujifunze!!!

Na King Chavala
MC/Sand Up Comedian
+255 713 883 797

Wednesday, July 24, 2013

KING CHAVALA......NINAWASHUKURU SANA KWA SUPPORT YENU NYOTE!!!

KING CHAVALA COMPLEX
SIO KWA AKILI WALA KWA UJUZI WALA UMAARUFU WALA ELIMU WALA VYOMBO VYA HABARI NA WALA SIO KWASABABU YA FEDHA,ILA MPAKA HAPA NIMEFIKA NI KWA NEEMA TU YA MUNGU!!

NINAMSHUKURU SANA MUNGU KWA KUWA RAFIKI MZURI KWANGU, SIJAFIKA BADO NINAKOKWENDA LAKINI SIKO PIA NILIKUWA, NINAPOKARIBIA KUTIMIZA MIAKA MIWILI YA "LAUGH AGAIN CONCERT SERIES-LACS" MNAMO NOVEMBA 20, NATAMANI NIANZE KUTOA SHUKRANI ZANGU ZA DHATI KABISA KWA KILA MTU ALIYE KARIBU NA MIMI NA ALINISAIDIA KWA HALI NA MALI MPAKA LEO NIMEFIKA HAPA.

AHSANTE KWA MICHANGO YA FEDHA NA MAOMBI NA BADO NAYAHITAJI SANA SANA HATA SASA....NINAWASHUKURU SANA WATU WA NGUVU AMBAO TUMEKUWA PAMOJA TANGU MWANZO HATA SASA!!!
INGAWA HATUJAFANYA TAMASHA LOLOTE MWAKA HUU,BASI TARAJIA MAMBO MAKUBWA DECEMBER 1

MUNGU AKUBARIKINI NYOTE MNAOJITOA KWA ROHO SAFI!!!

KING CHAVALA
+255 713 883 797
Facebook; King Chavala

YOUTH KINGDOM MINISTRIES NA SEMINA NYINGINE YA UONGOZI!!


HII NI NAFASI NYINGINE KWA KIJANA WA TANZANIA!
HII NI FURSA YA KIPEKEE YA KUIKIMBIA, MAANA HAUKUNA SABABU YA KUKOSA, JIFUNZE NA JIANDAE KIONGOZI WA KIFALME KATIKA ULIMWENGU WA ROHO!!
NI AUGUST 4, 2013 PALE DEAR MAMA HOTEL,DODOMA KUANZIA SAA SABA MCHANA MPAKA KUMI NA MBILI JIONI!
JIANDIKISHE SASA!! 0712 661842

AHSANTE MUNGU MAANA NAMIMI NITAKUWA MMOJA WA WAZUNGUMZAJI SIKU HIYO!!!

Thursday, July 18, 2013

BREEKING NEWS; AJALI MBAYA SANA YATOKEA HAPA DARAJANI RUAHA!!!

Mungu Wangu, Mungu wangu!!
Yaani madamu yametapakaa kila mahali dah!
Hii ni ajali mbaya sana kuwahi kutokea mwaka katika daraja hili aiseee!
Nakwambia ukiona picha huwezi kutamani kabisa kula nyamna!
Tisa wamekufa hapo hapo,tena wanne wamekatika vichwa na watatu wamevunjika miguu yote miwili na hawa wawili ndio Utumbo uko nje kabisa!
Hawa waliobaki hai ni zaidi ya Ishirini na tano lakini hali zao ni mbaya sana na yamkini tukawapoteza wengine ndani ya hizi siku mbili,hapa kila mmoja amechanganyikiwa na wengine wanajizungusha tu hapahapa huku wakilia na hamna wanachosaidia!
Namshangaa sana Mungu maana katika ajali hii kuna huyu mmoja tu, ambaye ni mdogo yeye ndio hajagugwa wala kuchubuliwa hata kidogo.
Naona Watu wengi wanakazana kusaidia kwa juhudi zote,
lakini wengi wanaogopa sana maana hali inatisha na kuna hatari ya wewe unaesaidia kupata majanga pia!
Ahsante Mungu kuna watu wamejiaminisha na hawaogopi hili awala lile na hawa wamesema hata wakiumia au kufa potelea mbali,bora wamejitoa kusaidia pale wanapoweza!
Na kwa mujibu wa Mashuhuda walioshuhudia ajali hii wanasema imesababishwa na mwendokasi wa dereva na ndio maana ikaleta madhara makubwa namna hii!
Yaani ni bonge la hasara,na kama ndio mtu alikuwa anaanza tu kujikwamua,atakuwa ameumia sana nafsini mwake,Jamani msiache kumuombea maana huwezi jua yanayomsibu!
Lakini pia nafikiri kama ile mikanda ingekazwa wala hayo yasingelitokea na inasemekana walijazwa humo kupita kiasi yaani....lakini watu tunakuwa na uchu wa fedha hivyo mpaka tunalazimisha hata idadi ikipitiliza sisi wala hatujali...ona sasa jinsi ajali hii ilivyoleta foleni,yaani magari ya huku hayaendi wala ya kule hayatembei na haijulikani tutavuka saa ngapi hapa!
Kweli imenisikitisha sana sana maana nasikia vilio tu vya majonzi vya hao waliobaki na unashindwa ufanye zaidi na wewe unashangaa machozi yanakutoka tu......Kwa habari zisizo rasmi nimesikia kuwa huyu dereva wa Lori alikuwa speed sana na aliporuka lile tuta basi tairi la mbele kulia likapasuka na hivyo likamvuta mpaka akaja akagonga ukingo wa kulia wa daraja na ndio hapo sasa lile Tenga waliokuwemo hao kuku likaruka mpaka mbele ya barabara na hivyo msleleko wa Trela ukaja ukapita katikati ya lile tenga kwa upana na ndio hapo wale kuku tisa wakafa vibaya palepale kama nilivyowalezea hapo juu....sasa jinsi lile trela lilivyokaka linaweza kuanguka wakati wowote ule maana linaning'inia juu ya daraja hivyo wananchi wanaogopa kama wakiingia kuwatoa wale kuku wazima linaweza kuwakuta la kuwakuta,na kijana mwenyewe inasemekana mtaji amekopa yaani hapa analia ile mbaya,lakini basi ndio ishatokea...pole yake kwa kweli...........
Babu: Wewe hebu zima hiyo Tv huoni kama mimi napumzika hapa,au wewe unapenda kusumbua tu watu.
(Babu alipoona huyu mjukuu hasikii akaamka na kumfuata,akamnasa bonge la kibao)
(YAANI BABU TU KUMNASA KIBAO YULE MJUU WAKE)
Akashtuka kumbe alikuwa anaota anaangalia Breeking news ya kwenye TV....Dah ndoto zingine bhana!!
****************************************************
(SAMAHANI JAMANI HIVI SCRIPT YA MOVIE IMEKAA VIZURI? TAFADHALI NAOMBA MAONI YAKO KWA AJILI YA MABORESHO)
— in Ruaha, Iringa.

Wednesday, July 3, 2013

.....HATA UFANYAJE HUWEZI KUWA KAMA MIMI!!!!

Habari yako rafiki yangu!!!
Natumai uko poa sana tu!


 
#....NAKUSHAURI TU KWA ROHO SAFI!!!!
Najua unaweza kufanya vingi sana ambavyo mimi nafanya, ndio tena zaidi hata ya mimi, tena unaweza kupata thawabu sana mbele ya macho ya watu kwa kufanya nifanyayo...ila kwa hakika huwezi kufanya kama mimi kwa kuwa wewe sio mimi na kamwe hautokuwa mimi na hata ukijitahidi namna gani utaishia kuwa wewe mwenyewe!!!


Na jinsi wewe ulivyo ni tofauti na uko  ambavyo hata mimi siwezi kuwa....kama unajaribu kujishindanisha na mimi basi mimi sio kipimio sahihi naam hata mimi kamwe siwezi kushindana na wewe.....kama ingewezekana wewe kufanya kile ninachokifanya basi kusingelikuwa na haja ya mimi kuwepo maana ningekuwepo kufanya nini hali kuna mtu anaweza kufanya kile nilichojia!?




Yamkini hata maamuzi yako mengi ni ya kufuata mkumbo,angalia kwanza wewe ni nani? una nini? na unatamani kufika wapi? na hapo ndio uanze kukazana kuyafikia malengo yako na sio vinginevyo!

Wengi wana dhana vichwani mwao,wanadhani kuna kuwa hai na baadae kuanza maisha...sikiliza hayo uliyonayo ndio maisha....ukisubiri kuishi kesho basi ujue utaishi peponi!!!


Na wengine wanaishi kwa woga sana,wanaogopa watu wanawaonaje au watasemaje na yamkini huumia kwanini hawana pesa au chakula....sikiliza huna haja ya kuogopa!!

WEWE ACHA MAISHA YA MAIGIZO,VAA UHUSIKA HALISI KISHA JIAMINI KATIKA HARAKATI ZAKO UONE KAMA TOFAUTI HAIONEKANI!!!
 
Utaanza kufanikiwa kama ukiwa halisi na ukiamua kuishi maisha yako,naam wewe wa wakati ujao ndio unapaswa kuwa mshindani wa wewe wa sasa....hakuna siku utaanza kuishi....ISHI SASA!!!


UKIACHA KUISHI KAMA WEWE NA KUANZA KUISHI KAMA YULE NA YULE NA IKIWA NA YULE ANAISHI KAMA YULE MWINGINE BASI WEWE NDIO KILAZA WA WOTE KWA IGIZO HILO.....Sasa hao wanaotaka kujifunza kwako wataona nini kwenye nafasi yako?


.......BE YOURSELF!!!!
+255 713 883 797
King Chavala-MC
Twitter @kingchavala
Facebook@King Chavala MC