 |
| King Chavala-MC & His Lovely Dady |

##@ HaPpY BiRthYdAy MR.ERASTO N.CHAVALA (King Chavala-Senior)@#
(**^^My Only and Lovely Biological Dady Au (Baba kwa msisitizo) i have hapa duniani!!!! Leo On 30th October!**@)))
Kuna jumapili moja hivi nilisema sana kuhusu MY Mama na nikaahidi kusema kuhusu Baba!
Mr.ERASTO NATHANAEL CHAVALA ni mtoto wa kwanza kati ya Watoto 11 wa
MR.NATHANAEL CHAVALA kama vile mama alivyo lango kwao, Miaka 8 kabla
Tanganyika haijapata Uhuru alishakuwepo duniani na Mungu alimsaidia kuwa
na akili sana,namaanisha akili sana kwa wakati wake,na hivyo
alibahatika kusoma vilivyo kabla Shetani hajamsumbua akikaribia kufanya
mtihani wa kidato cha sita,PCB ambapo aliumwa ugonjwa usioeleweka wa
tumbo kujaa maji na kuvimba kwa takribani miezi 3 na akapona wakati
imebaki wiki kadhaa kufanya mitihani ya mwisho (Inasemekana kuna watu
walikuwa wakimchezea na hawakupenda kusoma kwake),basi alimaliza shule
na matokeo yake hayakuwa mazuri sana kwasababu hiyo niliyoisema!
Alibahatika kujiunga na Jeshi kama ilivyokuwa ada kipindi hicho, na
kwasababu ya upekee wake walimsihi azingatie kuajiriwa na jeshi lakini
aligoma maana alikuwa na ndoto zake.
KUNA WAKATI ALIWAHI KATA KABISA
TAMAA YA MAISHA NA KUAMUA KUWA MLEVI SANA HUKU AKIWA ANATEMBELEA
PIKIPIKI....ILIWAHI KUTOKEA SIKU MOJA ALIPATA AJALI PALE DARAJANI
RUAHA-IRINGA NA AKABAKI AKINING'INIA, KIASI AMBACHO ILIKUWA ATANGULIE NA
PIKIPIKI IMFUATE JUU NA AFE KABISA....NA HAPO WALITOKEA WASAMARIA WEMA
KUMUOKOA,BADALA YA KUSHUKURU ALILAMIKA SANA NA KUFOKA...ETI KWANINI
WAMEMUOKOA NA YEYE ALITAMANI AFE TU....MUNGU ni mwaminifu sana maana
kila alipojaribu kujiua ilishindikana kwasababu ALIKUWA NA MAKUSUDI NA
YEYE, NA MUNGU KWA HAKIKA ALIJUA "The King Of Stand Up Comedy,A Star of
Africa" atatoka viunoni mwake!!!
....hapo baadae baada ya kujitambua
tena alijiunga na Chuo Cha Kilimo, Uyole Mbeya, na wakati huo kilikuwa
Chuo kweli kweli!! na baada ya kuhitimu alipangiwa Ileje na huko akawa
AFISA KILIMO WA WILAYA YA ILEJE....Na kwa kipindi hicho alikuwa mtu
mkali sana kwa wakulima wazembe na hali hiyo ilisababisha HALI YA KILIMO
NA MASHAMBA KUWA SAFI WAKATI WOTE na hivyo maendeleo kukua
sana...alifahamika kwa jina la "MUSUMULINGONDO"...Ingawa watu wengi
walikuwa wakimwita MSILINGONDO!!....na huku ndiko alikutana na Mama
akiwa anafanya kazi katika Hospitali ya Misheni-Kafule kama Mtaalamu wa
Maabara (Kazi anayoifanya mama yangu hata leo)
Kwasababu alikuwa
wakuja wengi walikuwa wakimuona kama sio mtu wa kawaida na kuna
incidence moja imewahi kutokea, ambapo Baba yangu amewahi kupoteza
Pochi(Wallet) ikiwa na mshahara wake wote na akatangaza sana wala
asijitokeze mtu,kumbe ilikuwa imeokotwa na Mzee mmoja ambaye alikuwa
anaogopwa mjini kwa Uchawi....basi siku ulitokea msiba na watu
wakajumuika,pamoja na Baba yangu,na wakiwa pale msibani alimuona mtu
anatoa pochi na akaitambua kuwa ni ya kwake...basi baba akamfuata na
kumuuliza,yule mzee akaakubali kuwa kweli aliiokota na pesa
alishazitumia na tangazo alilisikia....hivyo baba akabaki kujua ni
kwanini ameona vitambulisho na amesikia tangazo la upotevu na akakaa
nayo kimya...akabaki akiduwaa tu....MZEE HUYO ALIKUWA AKIJIAMINI SANA
KWA KUWA ALIKUWA ANAOGOPWA MNO!!!...Na wakati wa mazungumzo hayo chakula
kilikuwa tayari na Baba yangu aliombwa aondoke pale akale na
wenzake(KWANINI?) huyo mzee huwa anakulaga peke yake....Baba akagoma na
akasema nitakuwa hapahapa na huyu mzee,basi chakula kikaletwa na akaanza
kula,huko mgongoni yakaanza maneno ya hofu, wakimuhofia MSILINGONDO
kuwa yamkini nduio ikawa mwisho wa maisha yake...baada ya msiba hata
haukupita muda mrefu,wakati watu wanamuhofia Baba yangu,yule mzee
alifariki ghafla tu nyumbani kwake....sasa hapo ndio hadithi
ikageuka,YAANI KAMA MSILINGONGO AMEMMALIZA YULE MZEE ALIYEOGOPWA BASI
HUYO MSILINGONDO NDIO KIBOKO YAO!!!

Basi mama hakuishi kwa raha
hata kidogo,Baba aliomba uhamisho serikalini akanyimwa,akaomba tena na
tena na aliponyimwa kabisa akaamua kuacha kazi na kuamua kuhama kutoka
Ileje na kuja Mbozi na Maisha hapo yakaanza upya na amejenga hapo na
anaishi hapo hata leo!!
Baba yangu amechangia sana UTU NA
HEKIMA nilivyo navyo, ninampenda kwasababu alimpenda sana Mama pamoja na
maneno ya mashangazi ya kuudhi bado aliambatana nae kwasababu alijua
thamani ya Mama yangu,Baba yangu amewahi kuhukumiwa kufungwa jela mwaka
mzima kwa kosa la kugonga mtu na kuua bila kukusudia na wakati huo mama
yangu alikuwa mjamzito....ninampenda Baba yangu kwasababu sijawahi
kumuona hata siku moja akibishana ama kuzozana au kupigana na
mama,kwakweli sijawahi(Yaani hata kama kuna misundestandings huishia
chumbani).....Ninampenda Baba kwasababu ananipenda na amefanya kila
awezalo kuhakikisha mimi ninakuwa hivi nilivyo sasa!!
BAADHI YA MAMBO AMBAYO BABA YANGU AMENIACHIA,HATA SASA ANGALI YUPO NI HAYA;
1.Kwa baba kusoma ni lazima sio ombi,hata kusoma kuhusu Mungu na kanisa
haikuwa ombi,kula wala kuoga sio hiari yako ni lazima!! (BIDII NA
KUYAFANYA MAMBO YA MUHIMU KWANZA)
2.Baba hatoi pesa yoyote bila
mchanganuo unaoeleweka, kwahiyo unaweza pata pesa yoyote ile uitakayo
ikiwa tu unaweza kuitolea mchanganuo wake (ACCOUNTABILITY)
3.Baba
akisema jambo amelisema na akirudia ujue kuna adhabu juu yake....na
hakuna kazi utakayoifanya bila reward...yaani hata mtihani wa shule kuna
zawadi ya ukiwa kati ya 1-3 na kuna zawadi ukifeli!
4.Baba hachapi
kwa hasira na hachapi kabla ya mazungumzo na maelewano....yaani ukifanya
kosa ni mpaka mjadiliane na wewe ujue kweli hili kosa na mkubaliane
adhabu (NEGOTIATION) NA hata ukishaadhibiwa hakuruhusu uondoke machoni
kwake!
5.Baba hajawahi kuni-mislead kwenye maamuzi yangu na hata
kama ukitaka ushauri lazima akupe option uchague wewe,ingawa
nilipomaliza Form6 Tanga Tech alitaka kunishawishi kwa nguvu kusomea
Ualimu kwasabau ya Uchumi lakini niligoma na here i am,living and doing
what i love most!!!
6.Kila siku tukiwa pamoja Baba alikuwa na jambo
la kusema la kutujenga,kwa mfano alikuwa akisimulia hadithi,siku
nyingine alisoma neno,siku nyingine alitufundisha nyimbo na siku
nyingine alituletea filamu tuone...baba alinitembeza kwenye mashamba na
kunionyesha mipaka na kila maamuzi makubwa ndani ya familia hajafanya
bila kutushirikisha!!
7.Baba yangu amenisaidia sana sana kumpenda
Mungu na kuwa na msimamo wenye nidhamu maishani,amenisaidia sana kuwa
makini na maisha,kuelewa tafasiri nzuri ya maisha na kujua umuhimu wa
kuwasaidia wengine,zaidi amenifundisha sana KWA KUMPENDA MKE WAKE
SANA!!!
SIKU KWETU WOTE TUNAPENDA STORI NA KUCHEKA SANA,YAANI
TUKIONANA HUWA TUNACHEKA MNO....NAJIVUNIA BABA YANGU, NINAMPENDA
SANA....NIMETAMANI LEO NISEME KIDOGO KUHUSU BABA HUYU,KABLA SIJAANDIKA
KITABU KUHUSU FAMILIA YANGU!!
IKIWA LEO NI SIKU YAKO MUHIMU YA
KUZALIWA (BIRTH ANNIVERSARY), NATAKA ULIMWENGU WOTE UJUE KUWA BABA
NINAKUPENDA SANA SANA, NA NINAKUTAKIA MAISHA MAKAMILIFU....NATAMANI UONE
MKE NA WATOTO WANGU NA DAIMA SITAACHA KUJIVUNIA WEWE MAISHANI MWANGU!!!
KAMA WEWE NI RAFIKI YANGU NA UNANIKUBALI SANA ,BASI UJUE HUYU NDIYE
MHIMILI WA HIVI NILIVYO,SO USIACHE KUFANYA JAMBO KWA AJILI
YAKE....Unaweza kumuombea,unaweza kumsalimia,unaweza kumtumia text,vocha
au hata pesa na ukiwa karibu na Mbeya unaweza kwenda
kumsalimia.....HAPO ZIMEJAA HEKIMA NYINGI SANA!!!
Mwambieni akiwa
hai, mpeni salamu za pongezi, mtumieni furaha za mioyo yenu pamoja
nami......hii ni no. ya Baba yangu, naamini itatumika kwa heshima na sio
karaha wala ujinga
< 0715 470 526>
Ninawapongezeni nyote mnao-share birthdate na Baba yangu, hongereni pia sana, ninawajua wachache Jesus Up RaphaEl Angela,Ernest Kangajaka,Yulia Raymond,Faraji Nuru, Caroline Mwaipungu,Zaituni Siula na wengineo!!
SALAMU HIZI ZIJULIKANE KWA Hilda Chavala jamii hii yote!!!
THAT IS MY DADY, AND TODAY IS HIS HAPPY BIRTHDAY....I REAL ADMIRE AND LOVE HIM SO MUCH!!!!
Fredy E.Chavala!
+255 713 883 797