Thursday, July 23, 2015


KIMINI CHA MTOTO WA ASKOFU-Sehemu ya 1


UTANGULIZI;

Habari ndugu msomaji, ninaamini uko sawa na unayo afya ya mwili na akili. Kwa kuishi kwangu, japo kwa miaka hii michache ya ujana, kwa kuzunguka kwangu huku na kule, ndani na nje ya nchi na kwa kufanya kazi mbalimbali za ushauri wa biashara, kufundisha vijana, kufanya ucheshi wa kujitegemea (Stand Up Comedy), Ushereheshaji pamoja na Utafiti wa uwekezaji, nimekutana na kukumbana na mambo mengi sana ya kufurahisha na kuogofya, ya faida nay a kuyasikitikia,lakini kwa vyovyote vile yalivyo, yanafaa kwa fundisho na maonyo kwa jamii ya leo. Ndio maana mimi ninajiona nina wajibu wa ktumia vipaji vyangu, waledi na kalamu yangu kukushirikisha wewe yale yafaayo kukushirikisha ili kabla hujapatwa na lolote uwe umejifunza na kuonywa na wale yaliowakuta.

KIMINI CHA MTOTO WA ASKOFU ni simulizi halisi, ya mambo yaliyotokea katika maisha na simulizi inakusanya matukio halisi ama yanayosimamia ama kujengwa katika uhalisia. Hakuna hata tukio moja linalomlenga mtu moja kwa moja na wala hakuna Askofu ambaye binti yake ndio anatajwa humu. Ikitokea kuna sehemu ya simulizi hii inaonyesha kugusa au kuwiana na habari ya kweli ya mtu yeyote, basi ichukuliwe kama mfanano tu ama mgongano tu wa simulizi hii na matukio halisi!
Mimi Fredy Erasto Chavala ndio nimezungukwa na kukutana na haya katika simulizi hii, Nimegharimika, nimeumia na kujikuta katika maswaibu mengi na msingi wa haya yote ni kimini cha mtoto wa askofu, fuatana name sasa…..


Sehemu ya 1;

Nilitua uwanja wa ndege saa mbili na nusu ya usiku badala ya saa moja na dakika kumi, nah ii ilisababishwa na hali ya hewa kuwa mbaya na hivyo kulazimika kwenda kutua uwanja mwingine wa jirani kabla kurejea tena pale ambapo safari yetu ilikuwa inakusudiwa. Kutoka uwanja wa ndege mpaka mjini pana umbali kiasi, na hivyo ilinibidi aitha nichukue tax, bajaji au pikipiki, ama nitembee sana mpaka nje na kusubiri vibasi vidogo maarufu kama daladala, Lakini kwa bahati nzuri kuna mama mmoja aliyekuwa na watoto wawili na mizigo ambaye nilimsaidia wakati tunapanda ndege, na pia nikajikuta ninamsaidia tena wakati wa kushuka, huyu mama alikuja kuchukuliwa na mwenyeji wake na hivyo nikajipata kwenye lift ya gari hilo.

Siku hiyo ilianza kwa maluwe luwe maana dereva aliyekuwa ametumwa na mwenyeji wa yule mama, nadhani alikuwa amelewa ama alikuwa hajafudhu kukaa barabara kubwa, maana kilometa tatu kutoka uwanja wa ndege, alikuwa anataka kumtangulia mtu mbele na kukata kona kulia, kitendo hicho alikifanya kwa uzembe sana kiasi cha kumkwangua aliyekuwa mbele yake na ile kutaka kukata kona haraka mbele ya yule aliyemkwangua, tulijukuta tunagongwa ubavuni, mlango wa nyuma, tena sehemu ya mataa na hivyo kusababisha msongamano mkubwa sana wa magari. Gari tuliokuwa ilikuwa ndogo aina ya Verosa na ile iliyotugonga ilikuwa Toyota prado na humo alishuka dada mmoja ndani ya Viatu virefu na kimini cha bluu pamoja na blauzi iyoacha maziwa yake nje kidogo na miwani ya jua ikiwa hapo katikati ya mfereji inabembea, nwyele nyingi za kusukia na umbile matata sana. Alishuka kwa jazba na akaanza kutukana hapo kwa mdomo nay ale matusi ya mikono. Dereva wetu alikuwa akitetemeka sana na hivyo alikuwa hajibu kitu na mimi sikutoka nje haraka maana kesi ile ilikuwa hainihusu sana kama mgeni, lakini baada ya muda niliamua kutoka na kujaribu kuleta mwafaka kwa mabishano yale, basi nilipotoka na kuuliza tatizo ni nini hata jambo hili lisimalizike, ndipo yule dada alinigeukia kwa hasira sana, ninaamini alitaka kutamka tusi, lakini kwa bahati tu kugeuka kwake kuligongana na sauti moja nzito iliyotoka kwenye gari nyingine iliyokuwa inapita ikisema “Hey Rosemery Hujambo? Umepatwa na nini?” Basi aligeuka na kuwa mpole ghafla na nikamsikia akisema “Sijambo Mchungaji, Shikamoo! Bwana asifiwe?” Basi yule baba kama bahati tu tukagongana macho na japo sikumfahamu kwa haraka ila alinisalimia “King Chavala ni wewe? Au nimekufananisha?” Ni mimi mkuu! “Oh basi sawa, ninaamini jambo hilo litaisha vema, ninaamini katika hekima zako, kadi yangu hii hapa, Ninaomba tuwasiliane tafadhali!” Basi nikapokea ile kadi na kumuuaga na niliporudi kwenye tukio yule dada aliamua kuchukua namba za simu za yule mama, maana aliomba kulipa gharama za matengenezo, na basi yule dada akanitazama na ni kama alitamani kunisemesha jambo ila alijawa na aibu, maana alishajionyesha kama mshari na mkorofi na hapo ikajulikana kuwa ni binti wa kanisani. Aliamua kuondoka akiwa anajiuliza hivi mimi ni nani hasa niliyeshuhudia udhihirisho wa tabia yake ya kweli. Na mimi pia nikaamua kuwaaga wale ndugu na hivyo nikatafuta pikipiki hapo ikanipeleka mpaka mitaa ile ambapo nilikuwa na kazi kesho yake. Sikutaka kufikia kwa watu wala mbali sana na eneo nililoelekezwa kuwa ndio yatafanyika yale yaliyonileta katika mji huu.

Basi tulienda mpaka maeneo yale, nikafika mpaka ulipo ukumbi na hapo nikaachana na yule aliyenipeleka, hivyo ikanibidi nianze kuulizia maeneo hayo kama kuna hoteli ama mahali pa kufikia, hivyo nikaanza kuzunguka hapo mtaani kuona zilizopo, lakini mara nilijikuta kwenye mtaa Fulani ambao nilielekezwa hoteli moja hivi ambayo ilikuwa ni ghorofa na kwa maeneo hayo hiyo ndio ilikuwa na hadhi ya kujielewa, basi nikawa natembea kuelekea kwenye hoteli hiyo, nilipoikaribia hiyo hoteli nilishtuka sana maana yalisikika mayowe makubwa sana toka chumbani, na hakuna aliyekuwa na hakika haswa kunanini ama kuna nani humo ndani!
Nilisimama kwa muda nione kama watu wengine wanaopita wanasikia ninavyosikia ama ni mimi peke yangu ndio naona maluweluwe!

Ni ajabu na kweli kuwa kila aliyekatisha maeneo hayo,aligeuka huku na kule na kuendelea na safari,na wengine walionesha kama kusonya vile ama kupuuzia kana kwamba wamezoea kusikia!
Nimezoea kusaidia watu na hivyo hapa ikanipa tabu sana, nawezaje kwenda wakati kuna mtu anahitaji msaada? Basi nikabaki njia panda kama nisogee vile au nisimame au niondoke vile!
Kwakuwa nilikuwa mgeni maeneo hayo,basi nikaendelea na ile adhma ya moyoni mwangu ya kutafuta mahali pa kulala,na nilipomuuliza mama mmoja aliniambia kuna hoteli(lodge) tu maeneo haya,akasema "Ni hiyo hapo,ila zunguka kule mbele ndio kuna geti" basi nikaanza kujongea mbele na akili ikawa inanituma kuniambia nikiwa hapo nitajua siri ya makelele hayo!

Nimechoka sana na safari na natamani kupumzika aisee; Nikaona mlango wa mapokezi, nikatembea mpaka kwake, Nikamuuliza Kaka napata chumba,akadakia haraka "Poa kaka,karibu,nafasi zipo...Je unataka full au passport?" Mmh! Ndio nini sasa? "Namaanisha unataka usiku mzima au unaondoka muda sio mrefu?" Maswali gani hayo kaka ya kishenzi? Unaona nina begi,huwezi kuhisi mimi ni mgeni? Na unataka niondoke baada ya muda mfupi,Unaona nafanana na majambazi au Wanga? "Aah samahani kaka,basi keti hapo subiri wahudumu wakifanyie usafi fasta,Ni 30,000 tu" Nilikaa pale kando nikiwa nawaza,haya maeneo ni gani? Kwanza nimesikia mayowe na watu hawaonyeshi kuhali wala kusaidia na hapa napewa hadithi za kishenzi...ina maana hapa Chumba kinaandaliwa mgeni akifika tu au? Ama chumba kinaandaliwa kutokana na muda unaokaa,basi nikaendelea kusubiri!

Basi mara nikiwa kama nasinzia vile, nikashituliwa na yule mhudumu kaka tayari,naomba mfuate huyo dada akuonyeshe chumba hapo ghorofa ya pili,basi nikaainuka nakuanza kupanda,nikiwa napanda ngazi, nikapishana na mtu kama namfahamu vile,sijui ni nani! Ila nahisi ni mtu mmoja maarufu na yamkini nimewahi kumuona mahali,sema sina hakika sana yamkini nimefananisha maana alikuwa amevaa Kofia,wakati namwazia huku naendelea kutembea mara juu kabisa kwenye ile korido ya kuelekea chumbani kwangu,nikagongana uso kwa uso na binti mmoja aliyekuwa anajaribu kujifunika ili asifahamike akifika chini, na aliponiona akaishiwa pozi,nikasikia tu "Aaah Uncleee, Shikamooo,mambooo,Bwana asifiwe!" Sasa nikiwa bado nawaza huyu ni nani vile,basi nikatabasamu tu, na kusema Okeeeey Poa!
"Kaka chumba chenyewe ndio hiki" Alisema yule mhudumu,basi nikajikuta namwambia yule binti "Haya naona uko na yako, basi sawa..mimi ndio nimefika,nimeona nipumzike  hapa leo, Wewe uko chumba gani uncleee?"
Aaah Hapana mimi aaaah bye bwana!
Basi akashuka haraka akiwa kama amepaniki vile na mimi nikamwangalia akishuka chini na nikaangia ndani na kuweka mizigo yangu, Lakini mle chumbani nikagundua hakuna Taulo wala sabuni na nilipojaribu kupiga simu nikaona kama ni mbovu vile, nasi nikaamua nishuke chini,niombe taulo,sabuni,nichukue chakula na kulipa pia kuandika taarifa zangu pale mapokezi!
Basi wakati nashuka nikamkuta tena yule binti pale mapokezi akidai mzigo wake,sasa ikanibidi nipitilize kwanza kwenda wanakouza chakula,kisha nimalizie hapo...basi ninaporudi akawa ameshaondoka,Sasa nikiwa pale mapokezi nikamsikia yule kijana wa mapokezi akisema "Mabinti wengine jamani! Sijui wanakosa nini aisee?" basi nikadakia "Kwanini kaka?"

Basi akashusha pumzi na kusema "Kaka wewe acha tu,mambo mengine ni magumu sana kuamini ila hapa wanakuja Watumishi mbalimbali, wahubiri na hata waimbaji kadhaa wa injili na watu wengine maarufu,hapa ndio kijiwe chao....Na hata huyu binti aliyetoka hapa, Nasikia ni Mtoto wa..........ITAENDELEA!!


(c)King Chavvah, 2015
+255 713 883 797
Instagram; kingchavvah
Twitter @kingchavala